Jinsi ya kutumia jina moja Facebook


Indonesia ni nchi pekee iliyoruhusiwa watu wake kutumia jina mmoja kwasababu hawana majina mawili kama kwetu. Kwahiyo kama mtu haishi Indonesia ni ngumu kubadilisha jina mpaka utumie VPN.
VPN ni software inayokuwezesha kubadilisha muelekeo wa kifaa chako, kitasomwa kipo nchi fulani. Mfano Mimi nipo East Afrika kwahiyo nikutumia VPN nibadilisha Location na nitaonekana nipo UK, US au Indonesia.

VPN pia itakusaidia kuingia kwenye website au social media zilizozuiliwa kwenye nchi fulani. China hawaruhusu kutumia WhatsApp kwenye nchi yao kwahiyo hata ukifungua haitafanya kazi lakini ukitumia VPN utaweza kutumia WhatsApp ukiwa China.

Mahitaji
.
Download Indonesia VPN

Fuata hatua hizi ili uweze kutumia jina mmoja Facebook

1. Download  Indonesia VPV na install kwenye simu yako. Fungua App yako na  hakikisha simu yako imeunganishwa na Internet


2. Bonyeza Indonesia


3. Bonyeza Indonesia Jakarta


4. Bonyeza connect


 5. Baada ya ku-connect muonekano wa app yako utakuwa hivi


6. Ingia kwenye website ya Facebook au App ya Facebook. (mimi nishabadilisha tayari kwahiyo siyo tatizo). Bonyeza vimshale 3 juu kushoto mwa app yako ya Facebook.


7. Bonyeza kwenye kitufe cha language (hapo kwenye Bahama). Juu ya Free Basics


8. Chagua Bahasa Indonesia. Kisha bonyeza kitufe cha Back


9. Bonyeza kitufe cha Pengaturan (Settings)


10. Bonyeza Informasi Pribadi


11. Hapa lugha itabadilika itakuja kwenye lugha ya Kiingereza. Bonyeza kwenye Neno Edit.


12. Hapo utakuja ukurasa wenye majina yako. Andika jina mmoja kwenye first name or Surname, kisha weka password. kuthibitisha. Utakuwa umebadilisha jina lako. Rudi kwenye language badilisha lugha  na weka unayotaka.

Mpaka hapa Indonesia VPN haina kazi tena. Unaweza kuifuta/Kuinstall. Jina lako litabaki hivyo hivyo hata utumie kifaa gani kuingia facebook utakuta jina mmoja tu.

2 comments:

Note: Only a member of this blog may post a comment.